STAND UNITED YAIFUNZA ADABU SIMBA SC MJINI SHINYANGA ,MATOKEO YAKO HAPA

Mchezaji wa Stand Abasirim  Chidiebele aliyeipatia bao  kipindi cha kwanz-picha na Marco Maduhu-Shinyanga


Timu ya Stand United ya mjini Shinyanga imeinyuka club ya Simba bao moja kwa nunge katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara mchezo ulipopigwa jioni hii katika uwanja wa CCM Kambarage mjini Shinyanga.


Goli la Stand United (Chama la Wana) limefungwa na Abasirim  Chidiebele kipindi cha kwanza  mapema dakika ya 10 alifunga bao la kichwa kilichomshinda golikipa namba moja wa timu ya Simba Ivo Mapunda na kutinga moja kwa moja katika nyavu za goli la timu hiyo.

Katika mchezo huo ulioshuhudiwa na maelfu ya wapenzi wa soka kutoka Shinyanga na nje ya Shinyanga ulijawa na vituko vingi ambapo kabla ya mchezo huo shabiki mmoja wa timu ya Simba aliyefahamika kwa jina la  Rajabu Jota alikamatwa na mashabiki wa Stand United  akimwaga dawa katika mlango wa kutokea wachezaji wa timu ya Stand United.

Kitendo hicho kilisababisha mashabiki wa Stand kumchapa makofi na makonde kabla ya jeshi la polisi kufika eneo la tukio na kumchukua mtuhumiwa.

Baada ya mchezo kuisha kocha mkuu wa timu ya Stand Mathias Lure ameeleza kufurahishwa na matokeo hayo na kuahidi kuwa ataendelea kufanya mabo makubwa katika timu yake.

Kwa upande wake kocha mkuu wa Simba Golan Kuponovic amesema Stand siyo timu ya kubeza ni timu nzuri ndiyo maana wameshinda katika mchezo huo.

Stand sasa wanajiandaa kuikabili Kagera Sukari ambao wanatumia uwanja wa CCM Kambarage kama uwanja wao wa nyumbani wakiwa na pointi 18 nafasi ya 11 katika msimamo wa ligi hiyo ambapo Kagera wao wapo nafasi ya 3 wakiwa na pointi 25.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post