Maskini!! MREMBO HUYU AFARIKI BAADA YA KUBUGIA DAWA ZA KUPUNGUZA UNENE,ALIZINUNUA KWENYE MTANDAO!!

mama 2 

Ni binti mrembo wa miaka 21 aliyefikia Chuoni kimasomo ambapo alichukua maamuzi ya kununua dawa za kupunguza/kujikinga na unene alizozinunua kwenye mtandao (online).

April 12 2015 ndio ilikua siku yake ya mwisho duniani baada ya kulazwa hospitali na chanzo cha kifo chake kikiaminika ni hivyo vidonge ambavyo inasemekana vilikua na sumu.

Mama yake mzazi ameongea na kusema Madaktari wasingeweza kuokoa maisha yake, kunywa hizo dawa ni sawa na kujisogeza karibu na kifo, zinasababisha pia mwili upate joto kupitiliza na kusababisha pia ini kushindwa kufanya kazi.
Mama 1 
Eloise alipoanza kuona hali iko tofauti baada ya kunywa dawa alikwenda hospitali mwenyewe lakini ikawa imeshaharibu tayari, alichelewa kwenda.

Haikufahamika ni vidonge vingapi alimeza na alivitumia kwa muda gani lakini Polisi wa Uingereza wametoa onyo kwa yeyote mwenye mpango wa kununua dawa online aachane nao tena sanasana kupitia websites ambazo hazijasajiliwa.
mama 3

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527