Kumetokea ajali basi la Unique Express lenye namba za usajili T148 BKK likitokea jijini Mwanza kwenda Tabora kugongana na lori la kampuni la Cocacola katika kijiji cha Ibingo kata ya Samuye wilaya ya Shinyanga mkoani Shinyanga.
Watu 10 wamefariki dunia na majeruhi 50 wamekimbizwa katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga