ANGALIA PICHA- WAFUASI WA LOWASSA WATEMBELEA KITUO CHA WALEMAVU WA NGOZI (ALBINO) SHINYANGA

Wafuasi wa Lowassa wakiwa na watoto katika kituo cha Buhangija
Marafiki wa Lowassa wakiwa getini wakitafakari jambo kabla ya kuingia ndani-
Leo kikundi cha Vijana mkoani Shinyanga wanaouunga mkono harakati za waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa ikiwemo kuchukua fomu ya kugombea urais wametembelea kituo cha kulelea watoto wenye ulemavu wa ngozi(Albino)cha Buhangija Jumuishi katika manispaa ya Shinyanga na kushiriki shughuli za ujenzi wa jengo la huduma za afya linalojengwa na Wahindi ,kufanya usafi na kutoa msaada wa vitu mbalimbali ikiwemo chakula kwa ajili ya watoto 390 waliopo katika kituo hicho-Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog
Bango kubwa lililokuwa limebebwa na marafiki wa Lowassa( Friends of Edward Lowassa 4U Movement) wakiamini katika Umoja,Utumishi,Uwajibikaji na Uzalendo


Baada ya kuingia Kituoni-Marafiki wa Lowassa wakishiriki shughuli za ujenzi wa jengo la afya linalojengwa na Wahindi/wananchi

Marafiki wa Lowassa kupitia 4U Movement wakishiriki shughuli za ujezi,hapa wanachanganya zege

Wanaendelea na ujenzi

Wanachanganya zege

Kulia ni Afisa habari wa marafiki wa Lowassa mkoa wa Shinyanga Musa Jonas akishiriki shughuli ya ujenzi katika kituo cha walemavu cha Buhangija

Marafikiwa Lowassa mkoa wa Shinyanga wakifua nguo za watoto wanaolelewa katika kituo cha Buhangija Jumuishi mjini Shinyanga


Wafuasi/marafiki wa Lowassa wakifua nguo za watoto hao

Marafiki wa Lowassa wakifagia na kuchoma moto taka

Hawa wanaanika nguo baada ya kumaliza kufua
Zoezi la kufua nguo linaendelea

Miongoni mwa mabango yalikuwa yamebebwa na marafiki wa Lowassa

Marafiki wa Lowassa wakiwa wamebeba mabango

Mabango yalikuwa mengi

Mabango yakachukua nafasi zaidi

Wafuasi wa Lowassa wakiwa na watoto katika kituo cha Buhangija

Watoto wenye ulemavu wa ngozi,wasiosikia na wasioona

Kushoto ni Mwenyekiti/mratibu wa 4U Movement wilaya ya Shinyanga Ramadhan akizungumza katika kituo cha walemavu wa ngozi Buhangija mkoani Shinyanga


Mwenyekiti ambaye ni mratibu wa marafiki wa Lowassa mkoa wa Shinyanga Hassan Haruna akizungumza katika kituo hicho ambapo alisema wameamua kufika katika kituo hicho ili kuunga mkono jitihada zinazofanywa na serikali kupiga vita mauaji ya albino nchini na kuutangazia umma kwamba wanaamini kabisa kuwa kiongozi atakayeweza kuwatetea albino ni Edward Lowassa,kwani amefanya mambo mengi makubwa nchini,hivyo kitendo cha kukomesha mauaji haya itakuwa kazi rahisi kwake,hivyo kumshawishi achukue fomu ya urais muda ukifika.

Marafiki wa Lowassa wakijiandaa kukabidhi msaada wa
maharage,unga,mkaa,sabuni,chumvi,maji,soda,mafuta ya kujipaka na mafuta ya kupikia.

Zoezi la kukabidhi msaada linaendelea,kulia ni mkuu wa kituo cha Buhangija Peter Ajali akipokea mfuko wa unga

Kulia ni mkuu wa kituo cha Buhangija Peter Ajali akizungumza baada ya kupokea msaada kutoka kwa vijana hao

ambapo alisema hivi sasa kituo hicho kina watoto 390,kati yao wenye albinism ni 286,wasioona 40 na wasiosikia 64,na kwamba changamoto kubwa zaidi ni chakula kwani kwa mlo mmoja tu zinahitajika kilo  60 za unga,32 za maharage,70 mchele na nyama kilo 33,hivyo chakula kinahitajika--Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527