MCHEZAJI WA SIMBA SC AFARIKI DUNIA


Aliyekuwa kiungo wa timu ya Simba SC Christopher Alex Masawe amefariki dunia leo saa 3 Asubuhi katika hospitali ya Milembe mkoani Dodoma baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Kwa mujibu wa mama yake mzazi aliyekuwa akimuuguza, maziko yatafanyika keshokutwa siku ya Jumanne.

Christopher Alex atakumbukwa kwa kufunga penati ya mwisho katika mchezo wa Simba dhidi ya Zamalek na kuifanya Simba ifuzu hatua ya Robo Fainali ya michuano ya Klabu Bingwa barani Afrika mwaka 2003 mchezo uliopigwa nchini Misri.

Baadhi ya wachezaji waliounda kikosi hicho kilichoitoa Zamalek ni pamoja na Boniface Pawasa, Juma Kaseja na Suleiman Matola.

Rais wa Simba Evans Aveva ambaye yuko mjini Shinyanga katika pambano la ligi kuu dhidi ya Stand United ametuma salam za rambirambi kwa familia ya marehemu na kumuelezea marehemu kuwa aliitumikia Simba kwa juhudi, mapenzi na uaminifu mkubwa na kusema kwamba Simba itaungana na familia yake katika msiba huo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527