WAZIRI ATEKWA NYARA AKIWA HOTELINI

 
Wanamgambo wamemteka naibu waziri wa maswala ya kigeni katika serikali inayotambuliwa kimataifa nchini Libya.


Maafisa wanasema kuwa Hassan al Saghir alitekwa nyara kutoka chumba chake cha hoteli katika mji wa mashariki wa Al-Baida mapema jumapili.

Haijulikani ni kundi gani lililotekeleza kisa hicho.

Utekaji nyara umekuwa jambo la kawaida nchini Libya,ambapo serikali mbili zinapigania udhibiti huku makundi tofauti ya wanamgambo yakikabiliana.
 Via>>BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527