Mabosi na wafanyakazi wa kampuni hiyo wakiwa katika tambiko hilo linalodaiwa kufanyika wiki iliyopita.
Za
kitaa kutoka Mtwara zinadai kuwa bibi mmoja aliyeitisha Serikali kuwa
ikifanya mchezo na haki za watu wa mkoa huo atabadili gesi kuwa maji,
amewapigia tambiko Wafaransa wazungu wa Kampuni ya uchimbaji wa visima
vya mafuta ya Maurel et Prom (T) Ltd yenye
ofisi zake Chole Road, Msasani Peninsular, Dar es Salaam, baada ya kile
kilichodaiwa drill yao ya kuchimbia mafuta kukatika mara tatu wakati
wakichimba kisima cha urefu wa mita 3,000 chini ya bahari.
Inadaiwa
baada ya kuanza kuona maajabu katika kazi yao hiyo, fasta
walijisalimisha kwa bibi huyo huko Mtwara na kukubali kufanyiwa tambiko
ili mambo yanyooke, kama wanavyoonekana pichani hapo juu! Kama ni kweli,
basi bibi anatisha! Lol!!.
PICHA: Hisani ya Mtandao