Mtendaji wa kata ya Kakubilo Zefania Chembe akiwa ofisini kwake-Picha na Valence Robert-Malunde1 blog Geita |
Zefania alimwapisha mwenyekiti huyo ambaye hakuchaguliwa na wananchi kupitia kikao cha kamati tendaji ya kijiji cha Kikwete kilichofanyika Januari 23 mwaka huu.
Ngulu
alisimikwa kuwa mwenyekiti wa kitongiji hicho baada ya kuahirishwa kwa uchaguzi
wa serikali za mitaa uliofanyika Disemba 14 mwaka jana, kutokana na
kucheleweshwa kwa fomu za wagombea wa uenyekiti kutoka CHADEMA na CCM na hivyo
kutakiwa kusubiri baada ya siku 90 kwa mujibu wa sheria za uchaguzi.
Kufuatia
hali hiyo Viongozi wa Kata ya Kakubilo (UKAWA) waliiomba serikali itengue
mara moja uamuzi huo vinginevyo wanaandaa maandamano yasiyokuwa na kikomo
katika kata hiyo.
“Sisi kama viongozi wa Ukawa tunamuomba mkurugenzi atengue huu uamuzi wa kuapishwa kwa mwenyekiti huyu sisi pamoja na wananchi hatumtambui na tutaandamana kwa ajili ya hili”,alisema Abdallah Machimu ambaye ni katibu wa Ukawa kata ya Kakubilo.
Kwa upande
wa wananchi wa kitongoji hicho walimkataa mwenyekiti huyo na kudai kuwa
wao hawamtambui.
“Mwenyekiti
huyu aliyeapishwa na Mtendaji sisi hatumtaki kwa sababu hatukumchagua na wala
uchaguzi haukufanyika katika kitongoji chetu, sasa huyu bwana wamemtoa wapi
mbona tunafanyiwa mambo ya ajabu au kwa vile ni kijijini wanatufanya sisi
wajinga? Tunasema hatumtaki,’’walisema wananchi hao.
Malunde1 blog ilimtafuta mtendaji huyo kutaka kujua tuhuma hizo ni za kweli
ama ala, simu yake ya kiganjani iliita bila kupokelewa na badaaye kuzimwa.
Hivi
karibuni Chenge alituhumiwa na wananchi wa kijiji cha Kabayole kuhusika katika
ubadhirifu wa fedha za mradi wa chumba kimoja cha Darasa katika shule ya
msingi Kabayole baada ya kujenga darasa chini ya kiwango hivyo kulidanganya
baraza la madiwani la mwaka 2014 kuwa boma limekamilika wakati ni uongo.
Hayo yalibainishwa na wananchi wa kata hiyo wakishirikiana na viongozi wa Chama pinzani (CHADEMA) baada ya kugundua jengo la darasa hilo halijakamilika na liko chini ya kiwango.
Hayo yalibainishwa na wananchi wa kata hiyo wakishirikiana na viongozi wa Chama pinzani (CHADEMA) baada ya kugundua jengo la darasa hilo halijakamilika na liko chini ya kiwango.
Kufuatia taarifa
iliyopelekwa katika baraza la madiwani ya Januari 2014 na mtendaji huyo juu ya
kukamilika kwa mradi huo, ni ya uongo kwani jengo hilo lilikuwa bado
halijakamilika mpaka sasa.
Uchunguzi uliofanywa
kuhusiana na mradi huo umebainisha kuwa pesa nyingi kiasi cha Sh. Milioni 9 zimeorodheshwa
ambazo ni gharama za mradi kutumika, ambapo kiuhalisia kiongozi huyo amejilipa
mamilioni ya mradi huo, huku akilidanganya baraza la madiwani pamoja na
wananchi.
Kutokana na hali hiyo
wananchi wamepinga mradi huo na kumtaka mtendaji huyo arejeshe mara moja fedha
hizo na wameiomba serikali imfute kazi mtendaji huyo.
“Jamani sisi tunashangaa
tumechangishwa pesa, kwa kuuza kuku, bata, mbuzi pamoja na masufuria yetu…ili
tuchangie chumba hiki cha darasa lakini kiko chini ya kiwango na halijakamilika
sisi tulifikisha sh. Milioni tatu na serikali ilitoa sh. Milioni tisa
kukamilisha mradi huo,”alisema Joshua Juma.
Vilevile wananchi hao
waliendelea kumlalamikia mtendaji huyo , kwa kuwakamata kwa ajili ya kuchangia
maabara jambo ambalo walisema limekuwa kero kwao .
“Jambo jingine amekuwa
akitukamata tunapigwa na migambo wake na kubambikiziwa kesi kwa ajili ya
maabara tunanyanyasika kweli hatuna imani na mtendaji huyu, tunaishi kwa
mashaka ndani ya nchi yetu,”walisema wananchi hao.
Hata hivyo alipotafutwa na waandishi wa habari Chenge aligeuka mbogo na kutaka kuigeuza ofisi kuwa uwanja wa
masumbwi huku akiwatimua waandishi wa habari.
“Jamani sitaki kuwaona
,mmekuja kutafuta nini hapa nawaombeni mtoweke mara moja sina shida na nyinyi
na sitaki ugomvi na nyinyi waandishi”alisema Chenge.
Na Valence Robert-Malunde1 blog Geita