Mshauri wa masuala ya ulinzi katika Benki Kuu (BoT), Shaban Ndosi (39) amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashitaka ya kujaribu kumuua ofisa wa Polisi.
Ndosi alifikishwa mahakamani hapo jana na kusomewa mashitaka mbele ya Hakimu Mkazi Waliarwande Lema.
Wakili
wa Serikali, Janeth Kitali alidai kuwa Oktoba 21, 2014 katika eneo
daraja la Salender karibu na mataa ya kuongoza magari, alijaribu kumuua
askari Polisi, Koplo Salehe.
Hakimu
Lema alisema mshitakiwa hatakiwi kujibu mashitaka kwa kuwa mahakama
hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo na upelelezi umeshakamilika
hivyo kesi itahamishiwa Mahakama Kuu.
Mshitakiwa
aliachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya kuwa na wadhamini
wawili wa kuaminika waliosaini hati ya dhamana ya Sh milioni mbili pia
alitakiwa kuwasilisha mahakamani hati yake ya kusafiria. Kesi hiyo
itatajwa tena Februari 23 mwaka huu.