Kichochi alisema
Bongo Movie Shinyanga ambayo mwenyekiti wake ni Juma Ibrahimu Songoro maarufu
kwa jina la Songoro inalenga kuleta mabadiliko ya wasanii na umoja na maendeleo
Tanzania
Aliyataja
masharti ya anayetaka kujiunga uanachama Bongo Movie Shinyanga kuwa na sifa hizi:
Awe na akili timamu,awe anajua kuigiza,hakuna kigezo cha umri wala jinsia,awe
mhuzuriaji wa vikao vinavyoandaliwa na bongo movies,awe mwenye kujituma,awe
aliyetimiza haya masharti na kujaza fomu na kitambulisho,lakini pia awe na picha
tatu za paspot size na atimize gharama za usajili zifuatazo ikiwemo fomu ya
kujiunga,ada,na kiingilio vyote vikiwa na gharama isiyozidi shilingi elfu 30.
Ofisi zao zipo Ngokolo mjini Shinyanga karibu na Moleka Hotel ukifika hapo utaona Maandishi yanayosomeka Bongo Movies Development Organization(B.D.O) Shinyanga .TZ.Kama una kipaji Wasiliana nao kwa Email
Bongomovieshy05@gmail.com, au wapigie simu namba zinazosomeka hapo juu au chini au fika kwenye ofisi zao
|
Maandishi yanayosomeka kwenye ofisi za Bongo Movie Shinyanga
Katibu wa Bongo Movie Shinyanga Sophia Kichochi akizungumza na waandishi wa habari leo |
Picha ya pamoja baadhi ya wanachama wa Bongo Movie Shinyanga na waziri Membe wakati wa uzinduzi wa Bongo Movie Shinyanga jijini Mwanza tarehe 22/6/2014 |
Mwenyekiti wa Bongo Movie Shinyanga Juma Ibrahimu Songoro maarufu kwa jina la Songoro |