EMMANUEL OKWI AONGEZA MKATABA MWINGINE KUICHEZEA SIMBA

http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/2434166/highRes/818475/-/maxw/600/-/1450c9xz/-/okwi+clip.jpg

Kiungo mshambuliaji wa Simba, Mganda, Emmanuel Okwi, ameongeza mkataba wa kuichezea timu hiyo akisaini miaka miwili.

Awali, kiungo huyo mwenye kasi kubwa uwanjani, alisaini mkataba wa miezi sita ya kuichezea timu hiyo akitokea Yanga, akiondoka kwa mgogoro mkubwa.

Meneja wa kiungo huyo, Abdulfatah Saleh,alisema kuwa Okwi ameongeza mkataba huo baada ya kufikia makubaliano ya pande mbili kati yao na klabu hiyo.

Abdulfatah alisema, awali kiungo huyo alisaini mkataba mfupi wa kuichezea Simba ili kupisha kesi iliyopo kati yake (Okwi) na Yanga iliyomfungulia mashtaka kwa madai ya kukiuka makubaliano yaliyokuwepo kwenye mkataba.

Aliongeza kuwa, mara baada ya kumalizika kwa kesi hiyo iliyosimamiwa na Kamati yaSheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), ndiyo akaongeza mkataba huo mwingine.

“Okwi ameongeza mkataba mwingine wa kuichezea Simba, amesaini mkataba wa miaka miwili baada ya kesi yake na Yanga kumalizika kwa TFF kumruhusu kuichezea Simba kufuatia timu ya zamani kushindwa kutimiza makubaliano yaliyokuwepo kwenye mkataba wake.

“Mwanzoni alisaini mkataba wa miezi sita ili kupisha kesi hiyo imalizike, awali alisaini mkataba huo kwa hofu ya kushindwa kesi hiyodhidi ya Yanga,” alisema Abdulfatah.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527