Tahadhari!!! FAHAMU JINSI UNAVYOWEZA IBIWA ACCOUNT YAKO YA FACEBOOK KWA KUFUNGUA PICHA YA MWANAMKE ANAYEVUA NGUO AU ALIYE UCHI

Tafiti zinaonesha kuna idadi kubwa ya watu wanaotumia Facebook hubofya zaidi picha au video zinazoonesha matukio yanayoendana na ngono ama picha chafu.

 Lakini imebainika kuwa baadhi ya video hizo hutumiwa na hackers kuweza kuaccess taarifa za mtumiaji na kuteka akaunti yake.

Wataalamu wa masuala ya mitandao wa Uingereza wamewatahadharisha watumiaji wa Facebook na kuwataka kuwa makini na video zinazosambaa zikionesha msichana au mwanamke (hata kama wanamfahamu) akiwa anavua nguo na kuonesha kuwa ukibofya itakupeleka Youtube kuangalia video nzima.

Wameeleza kuwa video hizo hutuma taarifa zisizotegemewa kwenye browsers kwenda kwenye flash player na kisha kuiba taarifa za siri za mtumiaji.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527