RAIS MUGABE ATISHIA KUWAFUKUZA NCHINI KWAKE WANAOPIGIA DEBE USHOGA,ALIWAHI KUWATAJA MASHOGA KUWA WABAYA KULIKO MBWA NA NGURUWE

Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe, ametishia kuwafukuza kutoka nchini humo wanadiplomasia wanaopigia debe mapenzi ya jinsia moja.

Katika hotuba yake ya sherehe za kuadhimisha uhuru wa nchi hiyo, Mugabe alitumia fursa hiyo, kukaripia kile alichokiita upuuzi wa nchi za ulaya zinazohubiri ushoga.

Alituhumu nchi za ulaya kwa kukosa maadili na kusisitiza kuwa ndoa inaweza kuwa tu kati ya mwanamke na mwanamume.

Sio mara ya kwanza Mugabe amekemea suala la ushoga.
Aliwahi kuwataja mashoga kuwa wabaya kuliko Mbwa na Nguruwe.

Mapenzi ya jinsia moja ni haramu nchini Zimbabwe na mashoga hukamatwa mara kwa mara kwa kosa hilo
via>>bbc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments